Monday 12 December 2011

MAKAMU WA RAIS MGENI RASMI HAFLA YA KUUKARIBISHA MWAKA MPYA WA KIISLAM WA 1433.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya waumini na viongozi wa Jumuiya ya Kiislamu ya Istiqaama, baada ya kumalizilika kwa halfa hiyo Desemba 12.
Add caption
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba wakati wa halfa ya kuukaribisha mwaka mpya wa Kiislam iliyoandaliwa na Jumuiya ya Kiislam ya Istiqaama Tanzania Tawi la Dar es Salaam. Hafla hiyo ilifanyika Desemba 11, 2011 katika Ukumbi wa Karimjee jijini.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu wakati akiondoka kwenye Ukumbi wa Karimjee Dar es Salaam, Desemba 12, baada ya kumaliza shughuli ya hafla ya kuukaribisha mwaka mpya wa Kiislam iliyoandaliwa na Jumuiya ya Kiislam ya Istiqaama Tawi la Dar es Salaam.

Wednesday 7 December 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AHUDHURIA MKUTANO WA 17 WA MABADILIKO YA TABIANCHI DURBAN-AFRIKA YA KUSINI.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal,  akizungumza wakati wa mkutano wa majadiliano wa Viongozi wakuu 194 wa nchi wanachama  wa Itifaki wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya Tabianchi, juu ya kupunguza uzalishaji wa gesijoto Duniani kabla ya kuanza kwa mkutano mkuu wa 17 wa umoja huo uliofanyika jana Desemba 6 mjini Durban, Afrika ya Kusini.

Saturday 3 December 2011

MAKAMU WA RAIS ATOA RAMBIRAMBI KWA FAMILIA YA MAREHEMU DAVID WAKATI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitia saini katika kitabu cha maombolezo ya kifo cha aliyekuwa Mtangazaji wa TBC, David Wakati, alipofika nyumbani kwa marehemu huyo  Oysterbay jijini Dar es Salaam jana Desemba 2, kwa ajili ya kutoa mkono wa pole. Marehemu Wakati alifariki juzi jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitia saini katika kitabu cha maombolezo ya kifo cha aliyekuwa Mtangazaji wa TBC, David Wakati, alipofika nyumbani kwa marehemu huyo  Oysterbay jijini Dar es Salaam jana Desemba 2, kwa ajili ya kutoa mkono wa pole. Marehemu Wakati alifariki juzi jijini Dar es Salaam.

Friday 2 December 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AFUNGUA BARABARA YA NELSON MANDELA TEMEKE JIJINI DAR.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, DKt. Mohammed Gharib Bilal na Kaimu Balozi wa Umoja wa Ulaya, Enrico Strampeli, wakifunua kitambaa kwa pamoja ikiwa ni sehemu ya Ufunguzi wa  jiwe la Msingi la Barabara, wakati wa ufunguzi wa Barabara hiyo ya Mandela uliofanyika jijini Dar es Salaam, Desemba 2.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipanda mti wa kumbukumbu baada ya kufungua rasmi Barabara ya Nelson Mandela, uliofanyika Desemba 2, Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Kaimu Balozi wa Umoja wa Ulaya, Enrico Strampeli , wakikata upete kwa pamoja ikiwa ni ishara ya ufunguzi rasmi wa Barabara ya Nelson Mandela, uliofanyika leo Desemba 2, Temeke Jijini Dar es Salaam. Kulia kwa Makamu ni Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli na (kulia) kwa Balozi ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Meck Sadick.

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WATANZANIA WAISHIO BURUNDI

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza wakati alipokutana na Watanzania waishio nchini Burundi jana Novemba 30. Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Dkt. James Mwasi Nzagi (kulia) ni Mwenyekiti wa Kinamama wa Jumuiya ya Kinamama waishio Burundi, Siwajibu Hamis (wa pili kulia) ni Mwenyekiti wa Vijana wa Jumuiya hiyo, Mutalemwa Julian.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwaaga baadhi ya Watanzania waishio Burundi baada ya kumaliza mazungumzo alipokutana nao Bujumbura Burundi jana Novemba 30 na kuzungumzia mambo mbalimbali yanayoendelea katika Taifa la Tanzania.

Wednesday 30 November 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AFUNGA MKUTANO WA NCHI ZA MAZIWA MAKUU BUJUMBURA BURUNDI.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Balozi wa Tanzania, nchini Burundi, Dkt. James Mwasi, baada ya kuwasili kwenye ukumbi wa Golf  kwa ajili ya kufunga Mkutano wa Nchi za Maziwa Makuu, uliokuwa ukijadili Uendelezwaji wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika, uliomalizika jana Novemba 29, Bujumbura Burundi.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Makamu wa Rais wa Burundi, Therence Sinunguruza, wakati alipowasili kwenye ukumbi wa Golf  kwa ajili ya kufunga Mkutano wa Nchi za Maziwa Makuu, uliokuwa ukijadili Uendelezwaji wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika, uliomalizika jana Novemba 29, Bujumbura Burundi.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake ya kufunga Mkutano wa Nchi za Maziwa Makuu, uliokuwa ukijadili Uendelezwaji wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika, uliomalizika jana Novemba 29, kwenye Ukumbi wa Golf, Bujumbura Burundi.

Monday 28 November 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AFUNGUA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA SIKU YA VIONGOZI WA TAKUKURU-TANGA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akifungua rasmi Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Viongozi wa Takukuru Mkoani Tanga Novemba 28. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Takukuru, Edward Hosea (kushoto) ni Waziri wa Ofisi ya Rais-Utawala Bora, Mathias Chikawe.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Takukuru, Edward Hosea, wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Viongozi wa Takukuru, uliofanyika Mkoani Tanga leo Novemba 28. Kushoto ni Waziri wa Ofisi ya Rais- Utawala Bora, Mathias Chikawe.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa Takukuru.

Saturday 26 November 2011

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, ahudhuria Mahafali ya 23 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia Viongozi na wahitimu katika ngazi mbalimbali kwenye mahafali ya 23 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika tarehe 26 Nov 2011, Bungo Kibaha Dar es salaam.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA TAMASHA LA SIKU YA MTANZANIA LA WATU WA JAMII YA RUKWA NA KATAVI, JIJINI DAR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimsikiliza Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati akimpa maelezo kuhusu kinywaji cha kienyeji Pombe ya Chimpumu inayotumiwa na Kabila la watu wa Rukwa, wakati wa uzinduzi wa Tamasha la Siku ya Utamaduni wa Mtanzania iliyowasilishwa na Kabila la Jamii za Mikoa ya Rukwa na Katavi, lililofanyika kwenye Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam jana Novemba 25.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoka ndani ya nyumba ya asili ya watu wa Kabila la Wafipa, wakati wa uzinduzi wa Tamasha la Siku ya Utamaduni wa Mtanzania 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakitembelea mabanda ya maonyesho na kujionea Bidhaa za Vyakula vya asili vinavyotumiwa zaidi na watu wa Mikoya ya Rukwa na Katavi,Makamu wa Rais akikabidhiwa mkuki kama ilivyo katika mila za watu wa Rukwa na Katavi.

Saturday 19 November 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AZINDUA MAADHIMISHO YA MIAKA 10 YA UMOJA WA WABUNGE WA TANZANIA WA KUPAMBANA NA UKIMWI MJINI DODOMA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi zawadi ya picha Mwenyekiti wa Umoja wa Wabunge wa Tanzania wa kupambana na Ukimwi (TAPAC), Lediana Mng’ong’o, kwa kuwa mstari wa mbele katika kusimamia umoja huo, wakati wa uzinduzi wa Maadhimisho ya Miaka 10 ya Umoja huo tangu ulipoanzishwa. Uzinduzi huo ulifanyika kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa Mjini Dodoma, Novemba 18, 2011
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiinua Mshumaa juu baada ya kuuwasha ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Maadhimisho ya Miaka 10 ya Umoja wa Wabunge wa Tanzania wa kupambana na Ukimwi (TAPAC), uliofanyika kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa Mjini Dodoma, Novemba 18. Katikati ni Spika wa Bunge, Anne Makinda na Mwenyekiti wa Umoja huo, Lediana Mg’ong’o wakishangilia uzinduzi huo.

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AFUNGUA MDAHALO WA NAFASI YA UMUHIMU WA KATIBA KTK MAISHA YA WATANZANIA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akifungua Mdahalo wa Nafasi ya Umuhimu wa Katiba katika Maisha ya Watanzania, uliofunguliwa Novemba 17, katika Jumba la Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.

MAKAMU WA RAIS APOKEA MADAI YA WANANCHI KUHUSU MABADILIKO YA TABIA NCHI.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza wakati wa Kongamano la Msafara wa kuelekea katika mkutano wa mabadfiliko ya Tabia Nchi unaotarajia kufanyika Durban Afrika ya Kusini mwezi ujao. Kongamano hilo limefanyika Novemba 15, 2011 kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Thursday 10 November 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AONGOZA MAJADILIANO YA MKUTANO WA UWEKEZAJI WA CHAKULA NA KILIMO.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza wakati wa Mkutano wa Uwekezaji wa Chakula na Kilimo, ulioanza leo Novemba 10, 2011  kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza, jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano wa Uwekezaji wa Chakula na kilimo, baada ya kuongoza mkutano huo.

Wednesday 9 November 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL ASAINI TAMKO LA VIONGOZI WA DINI KUHUSU MABADILIKO YA TABIA NCHI.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisaini tamko la Viongozi wa dini kuhusu mabadiliko ya Tabia Nchi, wakati wa Tamasha la Vijana la ‘Tunaimani kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi’ lililofanyika kwenye Viwanja vya Don Bosco Upanga jijini Dar es Salaam leo Novemba 9, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya vijana hao kuelekea Durban kushiriki katika Mkutano wa 17 wa Mabadiliko ya Tabia nchi unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu, nchini Afrika ya Kusini. Kushoto ni Askofu Mkuu wa Jimbo la Tabora na Mwenyekiti wa Viongozi wa Dini Nchini, Askofu Paul Ruzoka. 
Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati wa Tamasha la wakati wa Tamasha la Vijana la ‘Tunaimani kuhusu Mabadiliko ya Tabia Nchi’.

Friday 4 November 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AFUNGUA MKUTANO WA MAWAZIRI WA WIZARA ZA MAENDELEO YA WANAWAKE NA WATOTO WA NCHI ZA MAZIWA MAKUU, JIJINI ARUSHA.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Wanawake na Watoto Zanzibar, Zainab Omar, baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Arusha, kwa ajili ya kufungua rasmi Mkutano wa Mawaziri wa Wizara za Maendeleo ya Wanawake na Watoto, wa Nchi za Maziwa makuu, ulioanza leo Novemba 4, katika Ukumbi wa Mikutano wa AICC jijini Arusha.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, DKt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na Mkuu wa Mkoa Arusha, Mulongo Magesa, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba na Balozi Liberata Mulamula, wakati akiingia kwenye Ukumbi wa Mikutano wa AICC.

Thursday 3 November 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AKUTANA NA MKURUGENZI WA MAZINGIRA, MAANDALIZI YA MKUTANO WA DURBAN.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Julius Ningu, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu Dar es Salaam leo Novemba 3, 2011, kuzungumzia maandalizi ya Mkutano wa 17 wa Nchi zilizoridhia mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya Tabia nchi unaotarajia kuanza mwishoni mwa mwezi huu  Durban Afrika ya Kusini. Kushoto ni, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais, anayeshughulikia mabadiliko ya Tabianchi, Richard Muyungi.

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA WAKURUGENZI WA TPDC NA TIC.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Mafuta nchini (TPDC), Yona Killagane, wakati walipokutana kwa mazungumzo Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu jijini Dar es Salaam Novemba 2, 2011. Kushoto ni Mkurugenzi Masoko na Uwekezaji wa Shirika hilo, Dismas Fuko.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Ujumbe wa Kituo cha Uwekezaji  Tanzania (TIC) wakati walipofika ofisini kwake jijini Ikulu Dar es Salaam, Novemba 2, 2011.

Wednesday 26 October 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AHUDHURIA MKUTANO WA MAWASILIANO WA KIMATAIFA GENEVA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika ufunguzi wa mkutano wa Mawasiliano wa Kimataifa, uliofanyika Oktoba 25, Geneva Switzerland, ambapo Tanzania ilikuwa ni moja kati ya nchi zilizoshiriki katika maonyesho ya mkutano huo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza katika mkutano wa Mawasiliano wa Kimataifa.

Saturday 22 October 2011

MAKAMU WA RAIS MGENI RASMI MAADHIMISHO YA KILELE CHA MIAKA 50 YA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati wa Kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam tangu kilipoanzishwa mwaka 1961. Sherehe hizo zimefanyika leo Oktoba 22, katika Ukumbi wa Nkrumah  Chuo Kikuu jijini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa Kitivo cha Sheria, baada ya kutoa tuzo kwa baadhi ya wanafunzi wa zamani wa Taaluma ya Sheria waliosoma katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Wednesday 19 October 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AHUDHURIA SHEREHE ZA KUMBUKUMBU YA KIFO CHA SAMORA MACHEL-MAPUTO

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,mkewe Mama Zakhia Bilal na Mama Maria Nyerere,wakiwa pamoja na baadhi ya Marais wa nchi za Afrika wakati walipohudhuria katika maadhimisho ya Kumbukumbu ya kifo cha aliyekuwa Muasisi na Rais wa Msumbiji, Samora Machel, zilizofanyika leo Oktoba 19, mjini Maputo Msumbiji.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na aliyekuwa mke wa Rais wa zamani wa Msumbiji, Mama Grace Machel, wakati walipokutana na katika viwanja vya Mozambique Heroes Square, kwenye sherehe za maadhimisho ya Kumbukumbu ya kifo cha muasisi wa nchi hiyo, Samora Machel, zilizofanyika leo Oktoba 19, mjini Maputo. Kulia kwa Makamu ni Mama Zakhia Bilal na (katikati) ni Rais wa Afrika ya Kusini, Jacob Zuma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Mohammed Gharib Bilal, akiteta jambo na Rais wa Afrika ya Kusini, Jacob Zuma.

Friday 14 October 2011

MAKAMU WA RAISI KATIKA SHUGHULI YA KUWASHWA KWA MWENGE WA UHURU.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Mwenge wa uhuru kiongozi wa mbia za mwenge huo mwaka 2011 2012 Mtumwa Rashid Halfan kutoka mkoa wa kaskazini Unguja, kwa ajili ya kuanza mbio za kukimbiza katika mikoa yote ua Tanzania baada ya kuuwasha rasmi leo katika kijiji cha Butiama Mkoani Mara.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka shada la mauwa kwenye Kaburi la Hayati Baba wa Taifa Mwalim Julius Nyerere baada ya misa maalum ya kumkumbuka muasisi huyo Taifa la Tanzania iliyofanyika leo kijijini kwake Mwitongo Butiama.

Thursday 13 October 2011

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA MAKAO YA WATOTO YATIMA, MSONGOLA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifunua kitambaa kuzindua jiwe la msingi la Kituo cha kulelea watoto Yatima na waishio katika mazingira magumu cha Full Gospel Children’s Home, kilichopo Msongola Wilaya ya Ilala Dar es Salaam. Hafla hiyo ya uzinduzi wa kituo hicho ulifanyika leo Oktoba 13, 2011
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa Kituo cha kulelea watoto Yatima cha Full Gospel Children’s Home
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika Picha ya pamoja na Viongozi wa Kituo cha kulelea watoto Yatima cha Full Gospel Children’s Home, kilichopo Msongola wilaya ya Ilala, baada ya kuzinduliwa kwa kituo hicho.

Wednesday 12 October 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL ATOA POLE MSIBA WA MTOTO WA MWAPACHU

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitia saini katika Kitabu cha maombolezo cha Harith Mwapachu, ambaye ni mtoto wa Balozi Juma Mwapachu, aliyefariki dunia jana Oktoba 11, 2011.Kulia ni Balozi Juma Mwapachu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mwenyekiti wa Chama cha (CHADEMA) Freeman Mbowe, wakati walipokutana katika msiba wa mtoto wa Balozi Juma Mwapachu.