Wednesday 11 July 2012

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AKUTANA NA UJUMBE KUTOKA SINCHUAN HONGDA GROUP KUTOKA CHINA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mwenyekiti aliyeongozana na ujumbe Kutoka Hongda Group ya Beijing China, Quan Zhezhu, wakati ujumbe huo ulipofiak ofisini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Julai 11, 2012 kwa mazungumzo. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Ujumbe Kutoka Hongda Group, Beijing China, wakati ujumbe huo ulipofiak ofisini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Julai 11, 2012 kwa mazungumzo. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

Monday 9 July 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL, AMPOKEA MAKAMU WA RAIS WA AFRIKA YA KUSINI ALIYEFIKA NCHINI KWA ZIARA YA SIKU MBILI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na kuzunguma jambo na makamu wa Rais wa Afrika ya Kusini, Kgalema Motlanthe alipokuwa akimpokea Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimpokea makamu wa Rais wa Afrika ya Kusini, Kgalema Motlanthe, aliyewasili nchini Julai 8, 2012 kwa ajili ya ziara ya siku mbili, ambapo atakuwa na mazungumzo na Makamu wa Rais Dkt. Bilal na kutatembelea Mazimbu mkoani Mororgoro. Picha na Muhidin Sufiani-OMR 

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL MGENI RASMI TUNZO ZA WASANII BORA 2012 WA MUZIKI WA ZANZIBAR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Tuzo ya Heshima msanii mstaafu wa muziki wa Taarab, Mwanacha Hassan Kijole (65) wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi za washindi wa Tuzo hizo za Wasanii bora wa muziki wa Zanzibar wa mwaka 2012, zilizodhaminiwa na Kampuni ya simu za mkononi ya Zantel.Hafla hiyo ilifanyika Julai 6, 2012 katika Ukumbi wa Hoteli ya Bwawani mjini Zanzibar. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Uzini na Mkurugenzi wa redio ya Zenji Fm, Mohamed Seif Khatib (kushoto) ni Mkurugenzi wa Biashara wa Kampuni ya Zantel, Zanzibar, Mohamed Baucha. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotub`a yake wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi za washindi wa Tuzo hizo za Wasanii bora wa muziki wa Zanzibar wa mwaka 2012,

Friday 6 July 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL, AMWAKILISHA RAIS JAKAYA KIKWETE KUONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI MJINI DODOMA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimwakilisha Rais Jakaya Mrisho Kikwete, kuongoza kikao cha  Baraza la Mawaziri, kilichofanyika leo mchana, julai 6, 2012 katika ukumbi wa TAMISEMI, mjini Dodoma. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

Friday 1 June 2012

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal amekutana na ujumbe wa Mfuko wa Dunia wa Kuhifadhi Maumbile (WWF) ambao umeelezea nia yao ya kutaka kushirikiana na Serikali ya Tanzania kuendeleza uvunaji endelevu wa raslimali asilia bila ya kuathiri mazingira.
Mkurugenzi Mkuu wa WWF James Leape ambaye alifuatana na ujumbe wa watu watano alimweleza Makamu wa Rais alipomtembelea ofisini kwake Ikulu jana, kuwa mara nyingi miradi inayohusiana na raslimali asilia ikiwemo ya madini inapotekelezwa husababisha uharibifu mkubwa wa mazingira katika eneo husika.
Alisema tathmini ya athari kwa mazingira ni muhimu ili kuendeleza uchimbaji endelevu wa madini hayo na kuiwezesha Tanzania kufanya vizuri katika kilimo na hivyo kufanikisha malengo yake ya kufikia uchumi wa kijani.
Katika mazungumzo hayo Makamu wa Rais alisema pamoja na matatizo yaliyopo lakini wakati miradi inapoanzishwa suala la tathmini ya mazingira huwa linapewa kipaumbele akitoa mifano ya miradi ya gesi asilia ya Songo songo pamoja na ya chuma na makaa ya mawe iliyoko Ludewa katika mkoa mpya wa Njombe.
Alisema serikali inaamini kwamba miradi hiyo itaharakisha maendeleo kwa kuwa itasaidia kufua umeme na hivyo kuwawezesha wananchi kupunguza matumizi ya mkaa kwa kupikia na pia kupitia mgodi wa chuma kuna fursa ya kujenga viwanda vya chuma kwa matumizi ya hapa nyumbani na kuuza nje ya nchi.
Aliuambia ujumbe huo kuwa suala la utunzaji wa mfumo wa ekolojia ni sera ya nchi na kusema asilimia 40 ya eneo la nchi limehifadhiwa kwa ajili ya faida ya kizazi cha sasa na kijacho.
Kuhusu uchumi wa kijani, Dk. Bilal alisema serikali imejipanga vizuri kwa hilo kwa kuwa tayari mikoa ya Iringa, Mbeya, Rukwa, Ruvuma na Morogoro inapewa uzito wa pekee kwenye suala la kilimo kwa lengo la kuiwezesha nchi kufikia uchumi wa kijani.
 
 

Wednesday 23 May 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA KITABU CHA ‘CHECKLIST OF TANZANIAN SPECIES.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati wa hafla ya uzinduzi wa Kitabu cha ‘Checklist Of Tanzanian Species’, iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Mei 22, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

Baadhi ya wadau waliohudhulia uzinduzi huo

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akionyesha Kitabu cha ‘Checklist Of Tanzanian Species’ baada ya  kukizindua rasmi kitabu hicho.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimsikiliza Meneja wa Shirika la TANBIF Node, Hulda Gideon, wakati alipotembelea sehemu ya maonyesho yaliyoandaliwa na Shirika hilo kwenye uzinduzi wa Kitabu cha ‘Checklist Of Tanzanian Species’

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika Picha ya pamoja na wadau waliohudhuria uzinduzi huo.

Monday 21 May 2012

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AFUNGUA MKUTANO WA SIKU NNE WA KUBADILISHANA UZOEFU BAINA YA SERIKALI YA TANZANIA NA CHINA KUHUSU MAFUNZO YA ULINZI.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal. Akisoma hotuba yake wakati akifungua mkutano wa siku nne wa kubadilishana uzoefu baina ya Serikali ya Tanzania na China, kuhusu mafunzo ya Ulinzi. Ufunguzi huo umefanyika leo Mei 21, 2012 katika Chuo kipya cha Jeshi National Defence College (NDC) kilichojengwa na Wachina eneo la Kunduchi jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea zawadi kutoka kwa Liutenant General wa Jeshi la Bangladesh, M F Akbar, baada ya kufungua rasmi mkutano.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea zawadi kutoka kwa Meja General Charles Lawrence Makakala.

Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wakiwa katika ukumbi wa mkutano wakati Makamu wa Rais Dkt Bilal, akifungua mkutano huo leo.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano huo mara baada ya kuufungua rasmi leo.