Wednesday 11 July 2012

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AKUTANA NA UJUMBE KUTOKA SINCHUAN HONGDA GROUP KUTOKA CHINA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mwenyekiti aliyeongozana na ujumbe Kutoka Hongda Group ya Beijing China, Quan Zhezhu, wakati ujumbe huo ulipofiak ofisini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Julai 11, 2012 kwa mazungumzo. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Ujumbe Kutoka Hongda Group, Beijing China, wakati ujumbe huo ulipofiak ofisini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Julai 11, 2012 kwa mazungumzo. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

Monday 9 July 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL, AMPOKEA MAKAMU WA RAIS WA AFRIKA YA KUSINI ALIYEFIKA NCHINI KWA ZIARA YA SIKU MBILI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na kuzunguma jambo na makamu wa Rais wa Afrika ya Kusini, Kgalema Motlanthe alipokuwa akimpokea Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimpokea makamu wa Rais wa Afrika ya Kusini, Kgalema Motlanthe, aliyewasili nchini Julai 8, 2012 kwa ajili ya ziara ya siku mbili, ambapo atakuwa na mazungumzo na Makamu wa Rais Dkt. Bilal na kutatembelea Mazimbu mkoani Mororgoro. Picha na Muhidin Sufiani-OMR 

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL MGENI RASMI TUNZO ZA WASANII BORA 2012 WA MUZIKI WA ZANZIBAR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Tuzo ya Heshima msanii mstaafu wa muziki wa Taarab, Mwanacha Hassan Kijole (65) wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi za washindi wa Tuzo hizo za Wasanii bora wa muziki wa Zanzibar wa mwaka 2012, zilizodhaminiwa na Kampuni ya simu za mkononi ya Zantel.Hafla hiyo ilifanyika Julai 6, 2012 katika Ukumbi wa Hoteli ya Bwawani mjini Zanzibar. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Uzini na Mkurugenzi wa redio ya Zenji Fm, Mohamed Seif Khatib (kushoto) ni Mkurugenzi wa Biashara wa Kampuni ya Zantel, Zanzibar, Mohamed Baucha. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotub`a yake wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi za washindi wa Tuzo hizo za Wasanii bora wa muziki wa Zanzibar wa mwaka 2012,

Friday 6 July 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL, AMWAKILISHA RAIS JAKAYA KIKWETE KUONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI MJINI DODOMA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimwakilisha Rais Jakaya Mrisho Kikwete, kuongoza kikao cha  Baraza la Mawaziri, kilichofanyika leo mchana, julai 6, 2012 katika ukumbi wa TAMISEMI, mjini Dodoma. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

Friday 1 June 2012

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal amekutana na ujumbe wa Mfuko wa Dunia wa Kuhifadhi Maumbile (WWF) ambao umeelezea nia yao ya kutaka kushirikiana na Serikali ya Tanzania kuendeleza uvunaji endelevu wa raslimali asilia bila ya kuathiri mazingira.
Mkurugenzi Mkuu wa WWF James Leape ambaye alifuatana na ujumbe wa watu watano alimweleza Makamu wa Rais alipomtembelea ofisini kwake Ikulu jana, kuwa mara nyingi miradi inayohusiana na raslimali asilia ikiwemo ya madini inapotekelezwa husababisha uharibifu mkubwa wa mazingira katika eneo husika.
Alisema tathmini ya athari kwa mazingira ni muhimu ili kuendeleza uchimbaji endelevu wa madini hayo na kuiwezesha Tanzania kufanya vizuri katika kilimo na hivyo kufanikisha malengo yake ya kufikia uchumi wa kijani.
Katika mazungumzo hayo Makamu wa Rais alisema pamoja na matatizo yaliyopo lakini wakati miradi inapoanzishwa suala la tathmini ya mazingira huwa linapewa kipaumbele akitoa mifano ya miradi ya gesi asilia ya Songo songo pamoja na ya chuma na makaa ya mawe iliyoko Ludewa katika mkoa mpya wa Njombe.
Alisema serikali inaamini kwamba miradi hiyo itaharakisha maendeleo kwa kuwa itasaidia kufua umeme na hivyo kuwawezesha wananchi kupunguza matumizi ya mkaa kwa kupikia na pia kupitia mgodi wa chuma kuna fursa ya kujenga viwanda vya chuma kwa matumizi ya hapa nyumbani na kuuza nje ya nchi.
Aliuambia ujumbe huo kuwa suala la utunzaji wa mfumo wa ekolojia ni sera ya nchi na kusema asilimia 40 ya eneo la nchi limehifadhiwa kwa ajili ya faida ya kizazi cha sasa na kijacho.
Kuhusu uchumi wa kijani, Dk. Bilal alisema serikali imejipanga vizuri kwa hilo kwa kuwa tayari mikoa ya Iringa, Mbeya, Rukwa, Ruvuma na Morogoro inapewa uzito wa pekee kwenye suala la kilimo kwa lengo la kuiwezesha nchi kufikia uchumi wa kijani.
 
 

Wednesday 23 May 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA KITABU CHA ‘CHECKLIST OF TANZANIAN SPECIES.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati wa hafla ya uzinduzi wa Kitabu cha ‘Checklist Of Tanzanian Species’, iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Mei 22, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

Baadhi ya wadau waliohudhulia uzinduzi huo

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akionyesha Kitabu cha ‘Checklist Of Tanzanian Species’ baada ya  kukizindua rasmi kitabu hicho.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimsikiliza Meneja wa Shirika la TANBIF Node, Hulda Gideon, wakati alipotembelea sehemu ya maonyesho yaliyoandaliwa na Shirika hilo kwenye uzinduzi wa Kitabu cha ‘Checklist Of Tanzanian Species’

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika Picha ya pamoja na wadau waliohudhuria uzinduzi huo.

Monday 21 May 2012

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AFUNGUA MKUTANO WA SIKU NNE WA KUBADILISHANA UZOEFU BAINA YA SERIKALI YA TANZANIA NA CHINA KUHUSU MAFUNZO YA ULINZI.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal. Akisoma hotuba yake wakati akifungua mkutano wa siku nne wa kubadilishana uzoefu baina ya Serikali ya Tanzania na China, kuhusu mafunzo ya Ulinzi. Ufunguzi huo umefanyika leo Mei 21, 2012 katika Chuo kipya cha Jeshi National Defence College (NDC) kilichojengwa na Wachina eneo la Kunduchi jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea zawadi kutoka kwa Liutenant General wa Jeshi la Bangladesh, M F Akbar, baada ya kufungua rasmi mkutano.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea zawadi kutoka kwa Meja General Charles Lawrence Makakala.

Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wakiwa katika ukumbi wa mkutano wakati Makamu wa Rais Dkt Bilal, akifungua mkutano huo leo.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano huo mara baada ya kuufungua rasmi leo.

Thursday 17 May 2012

MAWAZIRI WA ARDHI, MAZINGIRA WATOA TAARIFA YA ZOEZI LA BOMOA BOMOA NYUMBA ZA UFUKWENI NCHINI.

Kuelekea mchakato utakaoanza hivi karibuni wa kuendesha zoezi la bomoa bomoa ya nyumba ambazo zimejengwa kimakosa bila kufuata sheria na kanuni za ujenzi na makazi, na hivyo basi ujenzi huo holela katika maeneo ya ufukweni kumesababisha uharibifu wa mazingira ya fukwe hizo. Mawaziri wenye dhamana ambao ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Terezya Huvisa, wamekutana na Makamu wa Rais, Mhe. Gharib Bilal ili kujadili juu ya mwenendo na namna ya kulikabili zoezi hilo.

      Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, amekutana na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Terezya Huvisa, kwa mazungumzo na kupokea taarifa ya zoezi la Bomoa bomoa  nyumba zilizojengwa maeneo ya Ufukweni, ambalo linatarajia kuanza hivi karibuni.

 Mazungumzo hayo yalifanyika Ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu Dar es Salaam leo Mei 17, 2012. Katika picha kutoka (kushoto) ni Katibu wa Wizara ya Ardhi, Veldiana Mashingia, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka (kulia) ni Mkurugenzi wa Mazingira, Dkt. Julius Ningu na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dkt. Terezya Huvisa, baada ya mazungumzo hayo. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

Friday 11 May 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ATOA MSAADA KWA VITUO VIWILI VYA WATOTO YATIMA DAR.

 Msaidizi wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, eneo la Makaazi,
Peleleja Masesa (kushoto) akimkabidhi sehemu ya msaada wa vyakula, Mkurugenzi Mkuu wa
Kituo cha kulelea Watoto Yatima cha Orphanasi Trust Fund Msongola, Deusdelit Mitauto, kwa
niaba ya Makamu wa Rais, Dkt. Mohammed Gharib Bilal. Makabidhiano hayo yalifanyika jana jijini Dar es salaam.

Thursday 10 May 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA TAASISI YA WAKURUGENZI TANZANIA (IoDT)

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifunua kitambaa ikiwa ni ishara ya kuzindua rasmi Taasisi ya Wakurugenzi Tanzania (IODT),  wakati wa hafla fupi ya uzinduzi huo iliyofanyika leo Mei 10, 2012 kwenye Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi hiyo upande wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt. Mussa Juma (wa pili kulia) ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora) George Mkuchika na (kushoto) ni Mwenyekiti wa Taasisi hiyo, Pius Maneno. Picha na Muhidin Sufiani

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi zawadi ya Tuzo ya Heshima, Ibrahim Mohamed Kaduma,  kwa kuwa Mwanachama wa Heshima wa Taasisi ya Wakurugenzi Tanzania (IODT)

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma Hotuba yake wakati akizindua rasmi Taasisi ya Wakurugenzi Tanzania (IoDT)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja kwa kumbukumbu na Viongozi  na baadhi ya wadau walioshiriki katika hafla hiyo ya uzinduzi, baada ya kuzindua rasmi Taasisi ya Wakurugenzi Tanzania (IoDT) uliofanyika leo Mei 10 kwenye Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.

Tuesday 8 May 2012

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AZINDUA JUKWAA LA UCHUMI WA KIJANI LA SIKU 3 MKOANI IRINGA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akizindua rasmi Jukwaa la Uchumi wa Kijani, litakaloendelea kwa siku tatu Mkoani Iringa. Uzinduzi huo umefanyika leo Mei 8, 2012, katika Ukumbi wa Shule ya Msingi Mtakatifu Dominic Savio, mkoani Iringa. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo la Shule ya Msingi Mtakatifu Dominic Savio, baada ya kuzindua rasmi Jukwaa la Uchumi wa Kijani.

Wednesday 25 April 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AADHIMISHA SIKU YA MALARIA DUNIANI NA KUZINDUA RIPOTI YA MAFANIKIO A UTEKELEZAJI WA MIKAKATI YA MALARIA TANZANIA BARA.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akisoma hotuba yake wakati wa Kilele cha sherehe za maadhimisho ya Siku ya Malaria
Duniani, zilizofanyika leo Aprili 25, 2012 katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es
Salaam. Katika sherehe hizo pia Makamu wa Rais alizindua Ripoti ya utekelezaji wa mikakati ya malaria, Tanzania Bara.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akikata utepe, kuzindua Ripoti ya Mafanikio ya Utekelezaji wa Mikakati ya Malaria kwa
upande wa Tanzania Bara, wakati wa sherehe za maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Malaria
Duniani zilizofanyika kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo Aprili 25,
Katikati ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Haji Mponda (wapili kushoto) ni Kaimu
 mkuu wa Wilaya za Kinondoni, Temeke na Ilala, Jordan Lugimbana.
 

Monday 23 April 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASHIRIKI MAZISHI YA BRIGEDIA GENERAL MSTAAFU ADAM MWAKANJUKI UNGUJA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka mchanga katika kaburi la Brigedia General Mstaafu, Adam Mwakanjuki, wakati wa maziko yake yaliyofanyika kwenye Makaburi ya Mwanakwerekwe mjini Unguja, Aprili 22, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

Mnadhimu Mkuu wa Jeshi, Shimbo, akiweka mchanga katika kaburi la Brigedia General Mstaafu, Adam Mwakanjuki.
 Mke wa Marehemu Brigedia General mstaafu, Adam Mwakanjuki, Bi. Ikupa Mwakanjuki, akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu mumuwe, wakati wa mazishi yake yaliyofanyika kwenye makaburi ya Mwanakwerekwe mjini Unguja.

Wednesday 18 April 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA DINI LA WAISLAMU NA WAKRISTO JIJINI DAR.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya viongozi wa dini alipowasili kwenye Hoteli ya White Sands jijini Dar es Salaam,kwa ajili ya kufungua Kongamano la Dini la Waislam na Wakristo, lililoanza leo Aprili 18, 2012.

 Baadhi ya Viongozi wa Dini wakifuatilia kwa makini Hotuba ya Mgeni Rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, alipofika kufungua rasmi Kongamano la Dini la Waislam na Wakristo.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akifungua rasmi Kongamano .


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na baadhi ya Viongozi wa Dini.

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AFUNGUA MAONYESHO YA 7 YA ELIMU YA JUU YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati wa ufunguzi wa Maonyesho ya Vyuo Vikuu na Taasisi za Elimu na Utafiti yaliyoanza Aprili 18, 2012 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. 


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Akisikiliza maelezo kutoka kwa Mwalimu Simon Shayo, wakati alipotembelea katika Banda la Chuo Kikuu cha DUCE cha jijini Dar es Salaam, alipofika kuzindua maonyesho ya Vyuo Vikuu na Taasisi za Elimu na Utafiti yaliyoanza leo Aprili 18, 2012 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee. Kushoto ni Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa Chuo hicho, Abdul Njaid.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Akisikiliza maelezo kutoka kwa Makamu Mkuu wa Chuo cha Ardhi, Prof. Mangisen Kaseva, wakati alipotembelea katika Banda la Chuo hicho baada ya kuzindua maonyesho ya Vyuo Vikuu na Taasisi za Elimu na Utafiti yaliyoanza leo Aprili 18, 2012 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee. Kulia ni Ofisa Utawala  wa Chuo hicho, Rosemary Bundara. 


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja kwa kumbukumbu na baadhi ya wafanyakazi wa TCU.

Tuesday 17 April 2012

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL ASAINI KITABU CHA KUMBUKUMBU CHA KIFO CHA ALIYEKUWA RAIS WA MALAWI, DKT. BINGU WA MUTHARIKA LEO.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanania,Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisaini kitabu cha maomboleo ya aliyekuwa Rais wa Malawi, Dkt. Bingu wa Mutharika, katika Ofisi za Ubalozi wa Malawi nchini, zilizopo Mikocheni jijini Dar es Salaam, Aprili 17, 2012. Kulia ni Balozi wa Malawi nchini Tanzania, Flossie Asekanao Gomile-Chidyaonga. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MKUTANO WA 26 MWAKA WA PAMOJA KWA WADAU WA SAYANSI ULIOANDALIWA NA TAASISI YA TAIFA YA UTAFITI WA MAGONJWA YA BINADAMU (NIMR)

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Dkt. Mwele Malecela (watatu kushoto) kuhusu maonyesho ya wanasayansi yaliyoandaliwa  na Taasisi ya Taifa ya Utafiti ya magonjwa ya Binadam (NIMR) wakati alipofika kufungua mkutano wa 26 wa mwaka wa wadau wa sayansi ulioanza Aprili 16, jijini Arusha. Wa pili (kushoto) ni mke wa Makamu, Mama Zakhia Bilal na (kulia) ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Haji Mponda.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano wa 26 wa mwaka wa Wadau wa Sayansi  ulioandaliwa na Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR)

Makamu wa Rais Dkt. Bilal, akiwa katika picha ya pamoja kwa kumbukumbu na wadau wa Sayansi waliohudhuria mkutano huo wa 26 wa mwaka wa Wadau wa Sayansi jijini Arusha.

Monday 16 April 2012

MAKAMU WA RAIS AZINDUA BENKI YA ACB JIJINI ARUSHA LEO, AWEKA JIWE LA MSINGI.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake ya ufunguzi wakati alipokuwa akizindua rasmi jengo la Benki ya ACB jijini Arusha leo Aprili 16, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, na Mwenyekiti wa Bodi wa Benki ya ACB ya jijini Arusha, Dkt. Jonas Kipokola, wakifunua kitambaa kuashiria kuweka Jiwe la Msingi katika Benki hiyo mpya wakati Makamu alipofika jijini humo kuizindua rasmi leo Aprili 16, 2012. 


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja wa Benki ya ACB Tawi la Arusha, Anna Kavishe, kuhusu utendaji wa kazi na ramani ya jengo jipya la benki hiyo, baada ya kuizindua rasmi leo Aprili 16, 2012, jijini Arusha. Wapili (kulia) ni Mke wa Makamu Mama Zakhia Bilal na Kulia kwa Makamu ni Mwenyekiti wa Bodi wa Benki hiyo, Jonas Kipokola.

Friday 13 April 2012

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AZINDUA CHUO CHA UFUNDI STADI CHA VETA MKOA WA LINDI

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib
Bilal na Balozi wa Korea nchini, Young-Hoon Kim, wakikata utepe kwa pamoja kuashiria
uzinduzi rasmi wa Chuo kipya cha Ufundi Stadi cha VETA kilichojengwa Mkoa wa Lindi.
Uzinduzi huo ulifanyika jana Aprili 10, 2012. Kulia ni Mkurugenzi wa VETA, Zebadia Moshi.
Picha na Muhidin Sufiani-OMR
 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akibonyeza 'Alam', kuashiria uzinduzi rasmi wa Chuo kipya cha Ufundi Stadi cha VETA
kilichojengwa Mkoa wa Lindi.
 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib
Bilal, akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo la Chuo cha Ufundi Stadi cha VETA baada ya
kuzindua rasmi chuo hicho
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Ghariub Bilal,
akisikiliza maelezo kuhusu jinsi ya ufundishaji wanafunzi kwa kutumia mtambo wa kufua
Umeme, kutoka kwa Mwalimu wa Umeme Veta, Majolo Mwigole, wakati Makamu alipofika kuzindua chuo hicho