Tuesday 28 February 2012

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AANZA ZIARA YA MKOA WA IRINGA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka jiwe la Msingi katika Soko lililojengwa kwa nguvu za wananchi la Mfumbi, baada ya kuwasili Wilaya ya Makete kuanza ziara ya siku tatu mkoani humo jana Februari 27, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
 Makamu wa Rai wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipanda mti wa matunda wa kumbukumbu katika eneo la Chuo cha VETA cha Wilayani Makete mkoa wa Iringa, baada ya kuweka jiwe la msingi katika chuo hicho ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara yake ya mkoani Iringa jana Februari 27, 2012.

Saturday 25 February 2012

MAKAMU WA RAIS AZINDUA SOKO LA TUNDUMA LILILOUNGUA MOTO MWAKA JANA BAADA YA KUKARABATIWA UPYA.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuzindua Soko la Tunduma lililofanyiwa ukarabati baada ya kuungua moto mwaka jana, wakati akianza rasmi ziara yake ya kikazi katika Mkoa wa Mbeya jana Februari 24, 2012. Kushoto ni Mkewe Mama Asha Bilal, (kulia) ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro na (kulia kwake) ni Mbunge wa Mbozi Magharibi David Silinde.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwasili kwenye eneo la Soko la Tunduma jana Februari 24, 2012, kwa ajili ya kuzindua soko hilo baada ya kukamilika kwa ukarabati wake kufuatia moto ulioteketeza soko hilo mwaka jana. Makamu wa Rais amewasili mkoani Mbeya jana kwa ajili ya kuanza ziara ya kikazi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwahutubia wananchi wa Tunduma wakati alipofika eneo hilo kwa ajili ya kuzindua Soko la Tunduma baada ya kukamilika kwa ukarabati kufuatia soko hilo kuungua moto mwaka jana.

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AMALIZA ZIARA YAKE YA MKOA WA RUKWA NA KATAVI KWA KUZINDUA KAMPENI YA SUMBAWANGA NG’ARA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikabidhi vifaa vya kufanyia usafi kwa viongozi wa kampuni za kufanya usafi katika mitaa ya mjini Sumbawanga, wakati akizindua kampeni ya Sumbawanga Ng’ara  kwa ajili ya kudumisha usafi wa mazingira, ikiwa ni siku yake ya mwisho ya ziara yake katika mkoa wa Katavi na Rukwa jana Februari 24, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
  Makamu wa Rai wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuzindua Kampeni ya Sumbawanga Ng’ara yenye lengo la kudumisha usafi wa mazingira mjini Sumbawanga.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na Mama Asha Bilal (kushoto kwake) na Mkuu wa Mkoa wa Katavi na Rukwa, Eng. Stella Manyanya (kulia kwake) na baadhi ya viongozi wa mji wa Sumbawanga, mbele ya Sanamu la Sumbawanga Ng’ara baada ya kuzindua kampeni hiyo jana Februari 24, 2012.

Thursday 9 February 2012

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AKUTANA NA MABALOZI WA NORWAY NCHINI TANZANIA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akizungumza na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Ingunn Klepsivik, wakati alipofika Ofisini
kwake Ikulu Dar es Salaam,Februari 7, 2012 kwa mazungumzo. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
 
 

Monday 6 February 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AAGANA NA BALOZI WA CHINA NCHINI, LIU XINSHENG, ALIYEMALIZA MUDA WAKE

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi wa China nchini Tanzania, Liu Xinsheng, aliyefika ofisini kwake Ikulu Dar es Salaam leo Februari 6, 2012 kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake nchini. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea zawadi ya kitabu cha China kutoka kwa Balozi wa China nchini Tanzania, Liu Xinsheng, aliyefika ofisini kwake Ikulu Dar es Salaam leo Februari 6, 2012 kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake nchini.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AAGANA NA MABALOZI WATEULE WA TANZANIA NCHI ZA NJE IKULU DAR LEO.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na baadhi ya Mabalozi wateule wanaokwenda kufanya kazi nchi za nje walizopangiwa, wakati walipofika ofisini kwake Ikulu Dar es Salaam leo Februari 6, 2012 kwa ajili ya kumuaga kabla ya kwenda kuanza majukumu yao ya kikazi katika nchi walizopangiwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja kwa kumbukumbu na baadhi ya Mabalozi wateule baada ya kumaliza mazungumzo nao wakati walipofika ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam leo Februari 6, 2012 kwa ajili ya kumuaga kabla ya kuondoa kwenda kuanza majukumu yao ya kikazi katika nchi walizopangiwa.

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL APOKEA WANACHAMA WAPYA KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 35 YA CCM KIBAHA VIJIJINI.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi cheti, Katibu wa CCM wa Wilaya ya Mafia, Abdallah Mdimu, baada ya Wilaya hiyo kuibuka mshindi wa kwanza kwa ulipaji wa Ada za Wanachama, wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 35 ya chama hicho zilizofanyika Wilaya ya Kibaha Vijijini jana Februari 5, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea kadi ya mwanachama mpya kutoka CUF, Omar Said Hunda, aliyeamua kujiunga na CCM, wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 35 ya CCM.


Baadhi ya Wanachama wapya waliojiunga na Chama cha Mapinduzi CCM, wakila kiapo baada ya kukabidhiwa kadi zao za uanachama.