Thursday 3 November 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AKUTANA NA MKURUGENZI WA MAZINGIRA, MAANDALIZI YA MKUTANO WA DURBAN.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Julius Ningu, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu Dar es Salaam leo Novemba 3, 2011, kuzungumzia maandalizi ya Mkutano wa 17 wa Nchi zilizoridhia mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya Tabia nchi unaotarajia kuanza mwishoni mwa mwezi huu  Durban Afrika ya Kusini. Kushoto ni, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais, anayeshughulikia mabadiliko ya Tabianchi, Richard Muyungi.

No comments:

Post a Comment