Saturday 4 June 2011

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AIWAKILISHA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA MATAIFA YA TROPIKI YALIYO UKANDA WENYE MISITU MIKUBWA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwasili katika viwanja vya Bunge la Jamhuri ya watu wa Kongo jijini Brazzaville, jana Ijumaa, Juni 3, 2011 kuhudhuria Mkutano wa 3 wa Nchi za Tropiki zilizo katika ukanda wenye misitu mikubwa na mvua nyingi. Mkutano huo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka katika nchi zaidi ya 30 zilizo katika ukanda huo, mataifa yaliyoalikwa sambamba na mashirika ya Kimataifa yanayoshughulika na masuala ya mazingira. Picha na ofisi ya Makamu wa Rais.

No comments:

Post a Comment