Monday 13 September 2010

Kampeni siku ya leo Dodoma

Mgombea Mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal, akipokelewa na wanachama na wasanii wa ngoma za asili za Kabila la Wagogo, baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Mkoani Dodoma leo Sep 13 kwa ajili ya kuanza ziara yake ya mikutano ya  Kampeni baada ya mapumziko ya sikukuu ya Eid El Fitr, ambapo leo ameanza ziara hiyo katika Kanda ya Kati.( Picha na Muhidin Sufiani)

Wasanii wa Kikundi cha ngoma ya asili cha Maomanyika, wakiwa kwenye uwanja wa Makulu wakati wakimsikiliza Mgombea Mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal, alipokuwa akifanya mkutano wa Kampeni mkoani Dodoma leo Sept 13.



Mgombea Mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal, akihutubia katika mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Makulu mjini Dodoma leo Sept 13.

No comments:

Post a Comment